Rozari takatifu ni sala yenye nguvu na maarufu sana katika Kanisa Katoliki, husaliwa na wakristu kutafakari maisha ya Yesu na Maria yaani Fumbo la Ukombozi, hasa kipindi cha mwezi Mei na Oktoba. Inahimizwa kuisali kama familia kila siku. Tusali rozari tupate amani, wakosefu waongoke na wasiomjua Yesu Kristu wamjue na kuokoka.
Namna ya kusali Rozari.
Hatua ya
kwanza: Anza kusali Rozari kwa kuibusu miguu ya Bwana Yesu katika picha
yake Msalabani kisha fanya Ishara ya Msalaba gusisha msalaba huo kwenye paji la
uso, kifuani, bega la kushoto na kwa kutumia msalaba wa Rozari takatifu huku
ukiwa unasema
“Kwa
Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, Amina”.
Hatua ya
pili:Taja kwa ufupi nia ulizonazo. Tangaza nia hizo kwa sauti
kama mnasali wengi kwa pamoja, Mfano, unaweza kusema
“Tusali
kuombea amani katika nchi yetu na ulimwenguni kote" au tutolee rozari hii
kuwaombea wagonjwa wetu: au :tuwaombee wote walioomba tuwaombee" nk. Hiyo
ni mifano tu.”
Au
unaweza kutoa mambi kuendana na tendo lililotangazwa kwenye fungu husika la
tendo la rozari, au namna nyingine itakayofaa.
Hatua ya
tatu: Baada ya kufanya Ishara ya msalaba na kutoa nia za Rozari
yako, Sali sala ya Kanuni ya Imani:
Nasadiki
kwa Mungu, Baba Mwenyezi, mwumba mbingu na dunia. Na kwa Yesu Kristu, Mwanaye
wa pekee, Bwana wetu; aliyetungwa kwa Roho Mtakatifu, akazaliwa na Bikira
Maria, akateswa kwa mamlaka ya Ponsyo Pilato, akasulubiwa, akafa, akazikwa,
akashukia kuzimu; siku ya tatu akafufuka katika wafu; akapaa mbinguni; amekaa
kuume kwa Mungu Baba Mwenyezi; toka huko atakuja kuwahukumu wazima na wafu.
Nasadiki kwa Roho Mtakatifu, Kanisa takatifu katoliki, ushirika wa Watakatifu,
maondoleo ya dhambi, ufufuko wa miili, uzima wa milele. Amina
Hatua
ya nne: Baada ya kusali Kanuni
ya msalaba, kwenye punje kubwa ya Rozari inayofuata Sali sala ya Baba yetu:
Baba
Yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe; ufalme wako ufike, utakalo lifanyike,
duniani kama mbinguni. Utupe leo mkate wetu wa kila siku, utusamehe makosa
yetu, kama tunavyowasamehe na sisi waliotukosea. Usitutie katika kishawishi,
lakini utuopoe maovuni. Amina
Hatua ya
tano: Baada ya Sala ya Nasadiki pamoja na ya Baba Yetu, katika punje tatu za Rozari zinazofuata tunamwomba
Mungu (Utatu Mtakatifu) fadhila za Imani, Matumaini na Mapendo, zikiambatana na
Salamu Maria tatu.
Mojawapo
ya maneno yafuatayo hutumika:
“Mungu Baba utuongezee Imani.
Salamu
Maria, umejaa neema, Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote. Na Yesu
Mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria Mtakatifu, Mama wa Mungu, utuombee sisi
wakosefu, sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.
Mungu
Mwana utuongezee matumaini,
Salamu
Maria, umejaa neema, Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote. Na Yesu
Mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria Mtakatifu, Mama wa Mungu, utuombee sisi
wakosefu, sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.
Mungu Roho Mtakatifu washa nyoyo zetu kwa mapendo yako,
Salamu
Maria, umejaa neema, Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote. Na Yesu
Mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria Mtakatifu, Mama wa Mungu, utuombee sisi
wakosefu, sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.
Au;
“Utuongezee Imani ee Bwana,
Salamu
Maria, umejaa neema, Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote. Na Yesu
Mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria Mtakatifu, Mama wa Mungu, utuombee sisi
wakosefu, sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.
Utuongezee
matumaini ee Bwana,
Salamu Maria, umejaa neema, Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote. Na
Yesu Mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria Mtakatifu, Mama wa Mungu, utuombee
sisi wakosefu, sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.
Uwashe nyoyo zetu kwa mapendo yako ee Bwana,
Salamu
Maria, umejaa neema, Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote. Na Yesu
Mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria Mtakatifu, Mama wa Mungu, utuombee sisi
wakosefu, sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.
Hatua ya
sita: Katika Punje kubwa inayofuata baada ya punji ndogo tatu Sali
sala ya Atukuzwe Baba.
Atukuzwe
Baba, na Mwana na Roho Mtakatifu, kama mwanzo na sasa na siku zote, na milele,
Amina.
Hatua ya
saba: Tafakari juu ya fumbo la kwanza: Kila fungu la Rozari linahusishwa
na fumbo linalohusiana na maisha ya Yesu au Mama Bikira Maria. Anza na fumbo la
kwanza. Tafakari juu ya fumbo hilo na kisha usali Baba Yetu kwenye punje kubwa.
Hatua
ya nane: Ukiwa
umeshika Rozari, sali Salamu Maria mara kumi, yaani Salamu Maria moja kwa kila punje ndogo kumi za Rozari. Unaposali kila
Salamu Maria, zingatia fumbo ulilolitaja mwanzoni na utafakari umuhimu wake
unapoendelea kusali.
Hatua ya
Tisa: kwenye punje kubwa
inayofuata Baada ya Salamu Maria kumi, sali Sala Sala ya Atukuzwe Baba...... Kisha Sali sala
zifuatazo:
Tuwasifu
milele, Yesu, Maria na Yosefu,
Ee Yesu
wangu, utusamehe dhambi zetu, utukinge na moto wa milele, ongoza roho zote
mbinguni, hasa za wale wanaohitaji zaidi
huruma yako.
Hatua
ya kumi: Taja
fumbo la pili: Endelea na utaratibu kama wa hapo juu hadi kwenye fumbo
lifuatalo na urudie hatua ya 7 hadi hatua ya 9.
Hatua ya
kumi na moja: Endelea
na mafumbo yaliyosalia: Rudia hatua ya 7 hadi 9 kwa mafumbo yaliyosalia,
ukitangaza kila moja kabla ya kusali salamu Maria Kumi.
Hatua ya
kumi na mbili: Baada
ya kukamilisha miongo yote mitano, maliza Rozari kwa sala ya Salamu Malkia
(Salve Regina).
Salamu
Malkia, Mama mwenye huruma, uzima, tulizo, matumaini yetu, Salamu!
Tunakusihi ugenini hapa sisi wana wa Eva. Tunakulilia, tukilalamika na
kuhuzunika bondeni huku kwenye machozi. Haya basi Mwombezi wetu, utuangalie kwa
macho yako yenye huruma, na mwisho wa ugeni huu, utuonyeshe Yesu, Mzao
Mbarikiwa wa tumbo lako. Ee Mpole, ee Mwema, ee Mpendelevu, Bikira Maria.
Hatua ya
kumi na tatu: Maliza Rozari kwa kufanya Ishara ya Msalaba na
kusema, "Kwa jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu. Amina.
MATENDO
YA ROZARI
MATENDO
YA FURAHA (Jumatatu na Jumamosi)
Tendo la kwanza; Malaika Gabrieli anampasha habari Maria kuwa atakuwa Mama wa
Mungu.
Tumwombe
Mungu atujalie unyenyekevu.
Tendo la pili; Maria Mtakatifu anakwenda kumtembelea Elizabeti.
Tumwombe
Mungu atujalie mapendo ya jirani.
Tendo la tatu; Yesu anazaliwa Betlehemu.
Tumwombe
Mungu atujalie moyo wa ufukara
Tendo la nne; Yesu anatolewa hekaluni.
Tumwombe
Mungu atujalie usafi wa moyo.
Tendo la tano; Maria anamkuta Yesu hekaluni.
Tumwombe
Mungu atujalie kuwatii wakubwa wetu.
MATENDO
YA UCHUNGU (Jumanne na Ijumaa).
Tendo la kwanza; Yesu anatoka jasho la damu kwa ajili yetu.
Tumwombe
Mungu atujalie sikitiko la dhambi.
Tendo la pili; Yesu anapigwa kwa mijeledi kwa ajili yetu.
Tumwombe
Mungu atujalie kuacha dhambi za uchafu.
Tendo la tatu; Yesu anatiwa miiba kichwani kwa ajili yetu.
Tumwombe
Mungu atujalie kushinda kiburi.
Tendo la nne; Yesu anachukua Msalaba kwa ajili yetu.
Tumwombe
Mungu atujalie kuvumilia taabu.
Tendo la tano; Yesu anakufa Msalabani.
Tumwombe
Mungu atujalie kuwapenda Yesu na Maria.
MATENDO
YA UTUKUFU (Jumatano na Jumapili)
Tendo la kwanza; Yesu anafufuka.
Tumwombe
Mungu atujalie kugeuka watakatifu.
Tendo la pili; Yesu anapaa mbinguni.
Tumwombe
Mungu atujalie kwenda mbinguni.
Tendo la tatu; Roho Mtakatifu anawashukia Mitume.
Tumwombe
Mungu atujalie bidii katika dini yetu.
Tendo la nne; Bikira Maria anapalizwa mbinguni.
Tumwombe
Mungu atujalie kufa vizuri.
Tendo la tano; Bikira Maria anawekwa Malkia mbinguni.
Tumwombe
Mungu atujalie kudumu katika njia njema.
MATENDO YA MWANGA (Alhamisi)
Tendo la kwanza; Yesu anabatizwa Mto Jordani.
Tumwombe
Mungu atujalie uaminifu kwa ahadi zetu za ubatizo.
Tendo la pili; Yesu anageuza maji kuwa divai huko Kana.
Tumwombe
Mungu atujalie kuukoleza ulimwengu kwa chachu ya injili.
Tendo la tatu; Yesu anatangaza Ufalme wa Mungu.
Tumwombe
Mungu atujalie kupokea Ufalme wake kwa toba ya kweli.
Tendo la nne; Yesu anageuka sura.
Tumwombe
Mungu atujalie neema ya kuung’arisha ulimwengu kwa uso wa Yesu.
Tendo
la tano; Yesu anaweka Sakramenti ya Ekaristi.
Tumwombe
Mungu atujalie neema ya kujitoa sadaka kwa ajili ya wengine.
LITANIA
YA BIKIRA MARIA.
Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie
Kristo utusikie
Kristo utusikilize
Mungu Baba wa Mbinguni,…… Utuhurumie
Mungu Mwana Mkombozi wa dunia ……… Utuhurumie
Mungu Roho Mtakatifu …….. Utuhurumie
Utatu Mtakatifu Mungu Mmoja …….. Utuhurumie
Maria Mtakatifu ………. utuombee
Mzazi Mtakatifu wa Mungu …….. utuombee
Bikira Mtakatifu Mkuu wa Mabikira …….. utuombee
Mama wa Kristo ……… utuombee
Mama wa Neema ya Mungu ………….. utuombee
Mama Mtakatifu sana ……… utuombee
Mama mwenye usafi wa Moyo ……….. utuombee
Mama mwenye ubikira ……….. utuombee
Mama usiye na doa ……….. utuombee
Mama mpendelevu ………. utuombee
Mama mstajabivu ………. utuombee
Mama wa Muumba ………. utuombee
Mama wa Mkombozi ………….. utuombee
Mama wa Kanisa……….. utuombee
Bikira mwenye utaratibu ………….. utuombee
Bikira mwenye heshima ………….. utuombee
Bikira mwenye sifa ………….. utuombee
Bikira mwenye uwezo ………….. utuombee
Bikra mweye huruma ………….. utuombee
Bikra mwaminifu………….. utuombee
Kioo cha haki ………….. utuombee
Kikao cha hekima ………….. utuombee
Sababu ya furaha yetu ………….. utuombee
Chombo cha neema ………….. utuombee
Chombo cha kuheshimiwa ………….. utuombee
Chombo bora cha ibada ………….. utuombee
Waridi lenye fumbo ………….. utuombee
Mnara wa Daudi ………….. utuombee
Mnara wa pembe ………….. utuombee
Nyumba ya dhahabu ………….. utuombee
Sanduku la Agano ………….. utuombee
Mlango wa Mbingu ………….. utuombee
Nyota ya asubuhi ………….. utuombee
Afya ya wagonjwa ………….. utuombee
Kimbilio la wakosefu ………….. utuombee
Mtuliza wenye huzuni ………….. utuombee
Msaada wa waKristo ………….. utuombee
Malkia wa Malaika ………….. utuombee
Malkia wa Mababu ………….. utuombee
Malkia wa Manabii ………….. utuombee
Malkia wa Mitume ………….. utuombee
Malkia wa Mashahidi ………….. utuombee
Malkia wa Waungama dini ………….. utuombee
Malkia wa Mabikira ………….. utuombee
Malkia wa Watakatifu wote ………….. utuombee
Malkia uliyepalizwa Mbinguni ………….. utuombee
Malkia wa Rozari takatifu ………….. utuombee
Malkia wa amani ………….. utuombee
Mwanakodoo wa Mungu uondoaye dhambi za ulimwengu,… Utusamehe ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za ulimwengu,…. Utusikilize ee Bwana
Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za ulimwengu,.. Utuhurumie.
Utuombee, Mzazi Mtakatifu wa Mungu,…………..Tujaliwe ahadi za Kristo.
Tuombe
Ee Bwana Mungu, utujalie sisi watumishi wako afya ya roho na mwili siku zote;
na kwa maombezi matukufu ya Maria Mtakaatifu Bikira daima, tuopolewe na mashaka
ya saa, tupate na furaha za milele. Kwa Kristo Bwana wetu.AMINA
KUMBUKA.
KUMBUKA EE Bikra Maria mpole
sana, haijasikika kamwe kwamba ulimuacha mtu aliyekimbilia ulinzi wako,
aliyeomba msaada na maombezi yako. Kwa matumaini hayo, nakukimbilia, ee mama
mkuu wa mabikra nakuja kwako nasimama mbele yako,nikilalamika mimi mkosefu, ewe
mama wa Neno wa Mungu, Naomba usikatae maneno yangu,bali uyasikilize. AMINA.
0 Comments