Ibada
hii ilianza enzi za Kati lakini imepata umaarufu mpya kufuatia mafunuo ya
Bikira Maria yaliyoidhinishwa na Kanisa huko Kibeho, Rwanda mnamo miaka ya
1980. Katika mafunuo yake, Bikira Maria wa Kibeho aliwataka watu wasali Rozari
ya Mateso Saba ili kupata neema ya pekee ya toba.
Padre
Leszek Czelusniak, MIC, ambaye anahusika na misheni ya Maria huko Rwanda, alimhoji
Nathalie, mmoja wa walioona mafunuo ya Kibeho na kumwomba aeleze kwa kifupi
ujumbe wa Maria. Hivi ndivyo Nathalie alivyojibu:
"Bikira
Maria alisisitiza umuhimu wa sala. Alisema kwamba dunia ni mbaya. Ni lazima
kusali, kusali, kusali sana kwa ajili ya dunia hii ambayo ni mbaya, kusali kwa
ajili ya wenye dhambi, kusali kwa ajili ya toba yao. Alisisitiza sana umuhimu
wa toba: Geukeni kwa Mungu! Geukeni kwa Mungu! Geukeni kwa Mungu! Wakati
akisema kwamba watu hawaheshimu amri za Mungu, kwamba watu wana mioyo migumu,
pia alituomba tutafakari juu ya mafumbo ya Rozari na kuisali kila siku. Pia
alitufundisha Rozari ya Mateso Saba. Alituomba tuisali kila Jumanne na Ijumaa.
Alituomba tuwe watii kwa Kanisa, kumpenda Mungu kweli, na kumpenda jirani yetu kwa unyenyekevu
na unyofu. Alizungumza juu ya umuhimu wa kujinyima, roho ya toba na sadaka. Pia
alizungumza juu ya umuhimu wa mateso, kubeba mateso yetu kila siku. Alisema
kwamba hakuna mtu anayeingia mbinguni bila kuteseka. Pia alituambia kwamba
matendo ya upendo kwa maskini yanatufanya tuwe maua mazuri ambayo Mungu
anayapenda. Alitaka kanisa dogo lijengwe hapa Kibeho, ili kila mtu akumbuke matokeo
yake na kusali kwa ajili ya Kanisa na watawa. Bikira Maria alizungumza nasi kwa
Kinyarwanda kwa sauti yake laini sana."
Kuhusu Rozari
ya Mateso Saba, inatukumbusha kwamba Maria anafanya jukumu muhimu katika
Ukombozi wetu na kwamba aliteseka pamoja na Mwanawe Yesu ili kutuokoa. Rozari
hii inasaliwa kwa kutumia Rozari maalumu
ya Mateso Saba yenye mafungu saba yakiwakilisha mateso saba ya Maria na
kila fungu lina Punje saba.
Hivi
ndivyo Rozari hii inavyosaliwa:
Kila fungu moja la punje saba huanza na Sala ya Baba Yetu, kama ilivyo katika Rozari ya kawaida. Watu wengine huanza na Sala ya Kutubu, kwani ibada hii ni ya toba. Pia kama Rozari ya kawaida, makundi ya Salamu Maria saba ni fursa ya kutafakari juu ya "Mafumbo" - katika rozari hii, yafuatayo ni mateso saba;
1.
Teso la Kwanza
Unabii
wa Simeoni
Soma:
Luka 2:25-35.
Wakati
Maria na Yosefu walipomtoa mtoto Yesu hekaluni, Simeoni anatabiri kwamba
"upanga" (wa maumivu) utachoma roho ya Maria.
2.
Teso la Pili
Kukimbilia
Misri
Soma:
Mathayo 2:13-15.
Wakati
Mfalme Herode anaamuru kuuawa kwa watoto wote wa kiume wenye umri wa miaka
miwili au chini, Maria na Yosefu wanakimbilia Misri na mtoto Yesu.
3.
Teso la Tatu
Kupotea
Mtoto Yesu Hekaluni
Soma:
Luka 2:41-50.
Maria
na Yosefu wanamtafuta mtoto Yesu kwa siku tatu, hatimaye wanampata - baada ya huzuni kubwa -
hekaluni.
4.
Teso la Nne
Kukutana
Yesu na Maria kwenye njia ya msalaba.
Soma:
Luka 23:27-29.
Yesu anapoelekea Kalvari, amehukumiwa kusulubiwa, anakutana na mama yake, Maria. Yesu anaonekana akiwa amejeruhiwa, anatukanwa, analaaniwa na anadharauliwa na Maria anapata huzuni kubwa sana wakati akimuona Yesu akibeba msalaba wake mwenyewe kwenda mlimani kusulubiwa.
5.
Teso la
Tano
Kusulubiwa
kwa Yesu.
Soma:
Yohana 19:25-30.
Maria
anasimama karibu na Mwanawe anayekufa, akiwa hana uwezo wa kumhudumia anapolia
"Nina kiu." Anamsikia Yesu akiahidi mbingu kwa mwizi na kuwasamehe
maadui zake. Maneno yake ya mwisho, "Tazama mama yako," yanatuhimiza
kumtazama Maria kama mama yetu.
6.
Teso la Sita
Maria
anapokea mwili wa Yesu
Soma:
Zaburi 130.
Yesu
anashushwa kutoka msalabani na mwili wake unawekwa mikononi mwa Maria. Mateso
na kifo vimekwisha, lakini kwa mama yake, huzuni inaendelea. Anashikilia mwili
wake mikononi mwake.
7.
Teso la Saba
Maria
anashuhudia maziko ya Yesu
Soma:
Luka 23:50-56.
Mwili
wa Yesu unawekwa kaburini. Siku yenye huzuni kubwa zaidi katika historia
inaisha, Maria akiwa peke yake katika huzuni, akisubiri Ufufuo.
0 Comments