Machapisho yanayopendwa

6/recent/ticker-posts

ROZARI YA MATESO SABA.

 

rozari ya mateso saba


Ibada hii ilianza enzi za Kati lakini imepata umaarufu mpya kufuatia mafunuo ya Bikira Maria yaliyoidhinishwa na Kanisa huko Kibeho, Rwanda mnamo miaka ya 1980. Katika mafunuo yake, Bikira Maria wa Kibeho aliwataka watu wasali Rozari ya Mateso Saba ili kupata neema ya pekee ya toba.

Padre Leszek Czelusniak, MIC, ambaye anahusika na misheni ya Maria huko Rwanda, alimhoji Nathalie, mmoja wa walioona mafunuo ya Kibeho na kumwomba aeleze kwa kifupi ujumbe wa Maria. Hivi ndivyo Nathalie alivyojibu:

"Bikira Maria alisisitiza umuhimu wa sala. Alisema kwamba dunia ni mbaya. Ni lazima kusali, kusali, kusali sana kwa ajili ya dunia hii ambayo ni mbaya, kusali kwa ajili ya wenye dhambi, kusali kwa ajili ya toba yao. Alisisitiza sana umuhimu wa toba: Geukeni kwa Mungu! Geukeni kwa Mungu! Geukeni kwa Mungu! Wakati akisema kwamba watu hawaheshimu amri za Mungu, kwamba watu wana mioyo migumu, pia alituomba tutafakari juu ya mafumbo ya Rozari na kuisali kila siku. Pia alitufundisha Rozari ya Mateso Saba. Alituomba tuisali kila Jumanne na Ijumaa. Alituomba tuwe watii kwa Kanisa, kumpenda Mungu  kweli, na kumpenda jirani yetu kwa unyenyekevu na unyofu. Alizungumza juu ya umuhimu wa kujinyima, roho ya toba na sadaka. Pia alizungumza juu ya umuhimu wa mateso, kubeba mateso yetu kila siku. Alisema kwamba hakuna mtu anayeingia mbinguni bila kuteseka. Pia alituambia kwamba matendo ya upendo kwa maskini yanatufanya tuwe maua mazuri ambayo Mungu anayapenda. Alitaka kanisa dogo lijengwe hapa Kibeho, ili kila mtu akumbuke matokeo yake na kusali kwa ajili ya Kanisa na watawa. Bikira Maria alizungumza nasi kwa Kinyarwanda kwa sauti yake laini sana."

Kuhusu Rozari ya Mateso Saba, inatukumbusha kwamba Maria anafanya jukumu muhimu katika Ukombozi wetu na kwamba aliteseka pamoja na Mwanawe Yesu ili kutuokoa. Rozari hii inasaliwa  kwa kutumia Rozari maalumu ya Mateso Saba  yenye mafungu  saba yakiwakilisha mateso saba ya Maria na kila fungu lina Punje saba.

Hivi ndivyo Rozari hii inavyosaliwa:

Kila fungu moja la punje saba huanza na Sala ya Baba Yetu, kama ilivyo katika Rozari ya kawaida. Watu wengine huanza na Sala ya Kutubu, kwani ibada hii ni ya toba. Pia kama Rozari ya kawaida, makundi ya Salamu Maria saba ni fursa ya kutafakari juu ya "Mafumbo" - katika rozari hii, yafuatayo ni mateso saba;

 

1.        Teso la Kwanza

            Unabii wa Simeoni

            Soma: Luka 2:25-35.

          Wakati Maria na Yosefu walipomtoa mtoto Yesu hekaluni,     Simeoni anatabiri kwamba "upanga" (wa maumivu) utachoma      roho ya Maria.

2.      Teso la Pili

            Kukimbilia Misri

            Soma: Mathayo 2:13-15.

   Wakati Mfalme Herode anaamuru kuuawa kwa watoto      wote wa kiume wenye umri wa miaka miwili au chini,           Maria na Yosefu wanakimbilia Misri na mtoto Yesu.

3.      Teso la Tatu

Kupotea Mtoto Yesu Hekaluni

Soma: Luka 2:41-50.

Maria na Yosefu wanamtafuta mtoto Yesu kwa siku tatu, hatimaye wanampata - baada ya huzuni kubwa - hekaluni.

4.      Teso la Nne

Kukutana Yesu na Maria kwenye njia ya msalaba.

Soma: Luka 23:27-29.

Yesu anapoelekea Kalvari, amehukumiwa kusulubiwa, anakutana na mama yake, Maria. Yesu anaonekana akiwa amejeruhiwa, anatukanwa, analaaniwa na anadharauliwa na Maria anapata huzuni kubwa sana wakati akimuona Yesu akibeba msalaba wake mwenyewe kwenda mlimani kusulubiwa.

5.      Teso  la Tano

Kusulubiwa kwa Yesu.

Soma: Yohana 19:25-30.

Maria anasimama karibu na Mwanawe anayekufa, akiwa hana uwezo wa kumhudumia anapolia "Nina kiu." Anamsikia Yesu akiahidi mbingu kwa mwizi na kuwasamehe maadui zake. Maneno yake ya mwisho, "Tazama mama yako," yanatuhimiza kumtazama Maria kama mama yetu.

6.      Teso la Sita

Maria anapokea mwili wa Yesu

Soma: Zaburi 130.

Yesu anashushwa kutoka msalabani na mwili wake unawekwa mikononi mwa Maria. Mateso na kifo vimekwisha, lakini kwa mama yake, huzuni inaendelea. Anashikilia mwili wake mikononi mwake.

7.      Teso la Saba

Maria anashuhudia maziko ya Yesu

Soma: Luka 23:50-56.

Mwili wa Yesu unawekwa kaburini. Siku yenye huzuni kubwa zaidi katika historia inaisha, Maria akiwa peke yake katika huzuni, akisubiri Ufufuo.

Post a Comment

0 Comments