Karibu kwenye Blogu Yangu, NURU YA MARIA!
Naitwa JUSTINE BYABATO, mkatoliki na mwanafunzi wa Chuo
Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili.
Napenda kuona
jinsi imani yetu inavyoweza kuwa msukumo wa mabadiliko chanya katika maisha
yetu ya kila siku. Kama Mkatoliki, upendo wangu kwa Mama Maria unaniongoza
katika kuelezea kwa moyo jinsi tunavyoweza kushirikiana naye katika safari yetu
ya kiroho. Imani yangu inanipa nguvu na mwongozo, na ninafurahi kugawana safari
yangu na wewe.
Blogu yangu
inachipua kutoka moyo wangu wa Mkristo na mapenzi yangu kwa Mama Bikira Maria.
Ninapenda kuhamasisha wengine kushiriki ibada mbalimbali kwa Bikira Maria,
sala, na kujifunza jinsi tunavyoweza kufuata mfano wake kwa upendo na
unyenyekevu.
Karibu kushiriki nami katika NURU YA MARIA, ambayo ni sehemu ya kugundua mwanga wa imani yetu kupitia Mama Maria.
Asante kwa kuchagua kushiriki nami katika safari hii
ya kiroho inayomwelekea Mama Bikira Maria, mlinzi wetu na msaada wa kila siku.
Nuru ya Maria ni mahali pa kutafakari, kuelimishana, na kuguswa na uzuri wa ibada
zinazomuhusu Mama wa Mkombozi.
Katika blogi hii lengo langu kubwa ni kuhamasisha imani yetu
kupitia Mama Maria kwa kufanya yafuatayo;
1.
Ibada Za Bikira Maria: ninaangazia ibada mbalimbali
zinazomhusu Mama Bikira Maria na jinsi zinavyotuunganisha naye. Ninashirikisha sala mbalimbali za Bikira Maria, sala za Rozari, na matukio mengine yanayohusiana na ibada za Bikira Maria.
2 Matokeo ya Bikira Maria: Nuru ya Maria inaelezea
matokeo yote ya Bikira Maria katika
sehemu mbalimbali alizowahi kutokea hapa duniani. Tunashirikishana ushuhuda wa watu walioathiriwa na ibada za Mama Maria na jinsi imani yao
imeleta mabadiliko chanya.
3 Mafundisho ya Kiroho: Ninatoa mafundisho ya kiroho
yanayohusiana na Bikira Maria, kutusaidia kuelewa jukumu lake katika historia
yetu ya wokovu na njia zinazotuunganisha naye kiroho.
4 Safari yetu Kuelekea Mbinguni: Ninajadili njia za
kiroho na maadili yanayotufaa katika safari yetu ya kuelekea mbinguni. Kupitia
maandishi ya Blogi hii, ninajitahidi kuhamasisha na kuongoza kila
mmoja wetu kwa utakatifu kupitia msaada wa Bikira Maria
Ninakualika kushiriki: Ningependa kusikia kutoka
kwako! Jisikie huru kushiriki ushuhuda wako, au maswali yoyote unayoweza kuwa
nayo. Ninatamani Nuru ya Maria iwe mahali pa kujisikia karibu na kujengana
kiroho kwa msaada wa Mama Maria.
Asante kwa kuwa nami katika safari hii ya imani. Nipo hapa kukuza uelewa wetu wa Bikira Maria na kushirikiana katika upendo wa Kristo.
Kwa upendo wa
Maria,
Justine Byabato.
2 Comments
This comment has been removed by a blog administrator.
ReplyDeleteHakika naiona imani yangu ikizidi kuwaka kwa mapendo kwa HUYU MAMA MTAKATIFU WA MUNGU. Hata katika nyakati nisizoweza, pale ambapo nilikata tamaa kupindukia MAMA WA MUNGU Akaja kunifariji kwa kunipatia yale ambayo niliyaomba kwa MUNGU BABA NA BWANA YESU kupitia Jina la MAMA YETU BIKIRA MARIA. Hakika YEYE NI MAMA YETU pia Anatupenda kwa upendo ule wa ajabu kuweza kuelezea. Moyo wangu unajaa shukrani Kwake. Aksante sana kaka Justine kupitia haya machapisho unanifanya nijiskie amani na furaha zaidi ya Kumtangaza MAMA WA MUNGU hata pale napokutana na upinzani kutok kwa baadhi ya watu wasiotambua bado umuhimu mkubwa sana Aliopo Nao MAMA WA MUNGU. Naamini nitatumia pamoja na hizi makala zako kuwajulisha watu juu ya MAMA MARIA na namna Anavotupenda na kutuombea daima.
ReplyDelete" Pumziko la Milele uwape ee BWANA na mwanga wa Milele Iwaangazie wapumzike kwa amani. Amina.