Kanisa
linafundisha kuwa Roho hutoka Toharani punde tu zinapokamilisha kusafishwa kwa moto. Toharani
sio moto wa milele, ambapo Roho haiwezi kutoka. Ukiwa umezungukwa na moto
unaofika ndani ya Roho yako, maumivu gani
unayoyapata! Moto wa kawaida unaunguza miili tu, Fikiria kwa jinsi gani
moto wa toharani unavyokuwa nani anaweza kushika kaa la moto mkononi kwa dakika
moja? Lakini moto wa toharani unashika Roho; unafika katika akili kumbukumbu na
fahamu. Nani awezaye kustahimili moto huo?. Inasafisha Roho bila hata
kuhiaribu.
Moto wetu si chochote ukilinganisha na ule wa
toharani. Moto wa ulimwengu huu ni zawadi kutoka kwa Mungu, Moto wa Toharani
uliumbwa kwa haki yake, moto wa toharani ni sawa na ule wa moto wa
milele, isipokuwa mda wa kukaa huko ndio utofautiana, maumivu ya dunia hii hayawezi kulinganishwa na yale ya toharani.
Nani atakataa kusikia maombolezo yao? Fikiria
kuwa kama ungekuwa huko na hakuna mtu
anayeonesha upendo kwako, unawezaje kuuona
ukatili huo? Fikiria vizuri kuhusu ili na chukua hatua.
Mfano:
Stanislasi Kostka, Mjesuit kutoka Polandi,
aliona Roho ya toharani ikiwa imefunikwa
kwa miale ya moto na ilikuwa ikipiga mayowe. Stanislasi aliuliza Roho hiyo kuwa
moto huo ni kama wa duniani?. Roho
ilijibu kuwa moto wa duniani unapoulinganisha na moto wa Toharani, moto wa
duniani ni kama jiwe laini la thamani. Haikuwa rahisi padri kuamini, padri
Stanislaus alimwambia kuwa alikuwa anatoka kuonja kidogo moto huo, kama
inawezekana.
“Ah! Mwanadamu aliyebado duniani hawezi kuhisi
hata chembe ya moto huo. Lakini kama unataka kujua, nipe mkono wako nami nikuoneshe”
ile roho ilisema.
Stanislas alipanua mikono yake ile Roho
ilimwangushia tu tone la jasho lake wala haikumshika. Alipata maumivu makubwa Stanislas
alipiga kelele kiasi kwamba alikuwa anataka kufa kwa haraka marafiki zake
walikuja na aliwaeleza kilichotokea.
Wote waliogopa na kuchukua maamuzi ya kuongeza
toba, kuachana kabisa na anasa za dunia hii, pamoja waliamua kumwambia kila mtu
kuhusu moto wa toharani, ili watu waweze kujifunza jinsi ya kuepuka toharani.
Mtakatifu Stanislas aliishi mwaka
mmoja zaidi akiwa na maumivu makali ya jeraha alilopata ambalo alikuweza
kupona.
Padri Ferdinand wa Castile alilipoti
ukweli mwingine wa tukio lililotokea
katika nyumba ya watawa., huko nchini uhispania.
Katika Konventi hiyo kulikuwa na mapadri
wawili waliokuwa marafiki, na walipenda sana kuongea kuhusu mambo mbalimbali. Waliahidiana kukumbukana iwapo
wakifa.
Mmoja wao alifariki, na dakika chache baada ya
kifo chake padri huyo alimtokea rafiki
yake baada ya kumsalimu, alimwambia rafiki yake kuwa anateseka sana kwa mda
mrefu kwa sababu ya kosa dogo sana ambalo hakulilipia akiwa hai ili kumfanya
rafiki yake amsaidie, alimwonesha miale ya moto, ambayo ilikuwa ikimtesa alisema “Hakuna kitu chochote duniani kinachoweza kukuelezea
vizuri kuhusu moto huu. Je unataka nikuoneshe?” Roho hiyo iliweka mkono wake katika meza cha kushangaza
mkono huo ulitoboa meza na kuzama
chini.
Meza hiyo ambayo ni ushahidi wa moto wa
toharani imetunzwa huko Zamora
uhispania.
Mungu anaweka Roho katika moto hadi inaposafishwa
kabisa. Roho inapomalizia kusafishwa roho hiyo hukaa mbele ya Mungu na
inaunganika na Mungu Roho hapo haiwezi tena
kuteseka bali inahisi moto wa mapendo ya Mungu.
0 Comments