Machapisho yanayopendwa

6/recent/ticker-posts

HAKUNA NOELI BILA BIKIRA MARIA




Bila 'fiat' ya Maria (neno la Kilatini linalomaanisha idhini), tusingekuwa tunasherehekea Krismasi au historia ya wokovu ingekuwa imeandikwa upya. Ndiyo jinsi jukumu muhimu la Mama Maria lilivyokuwa.

Kujua mapenzi ya Mungu si rahisi kama ilivyokuwa kwa kupashwa kwake  Maria kuliko kuwa na msisimko. Alipokubali mapenzi ya Mungu, alipitia vikwazo na majaribu mbalimbali, ingawa alikuwa mama wa Masihi. Kwa mfano, alipojifungua Yesu, hakukuwa na nafasi inayopatikana katika nyumba ya wageni. Aliridhika kumzaa mwana wake ndani ya hori ambapo wanyama walikuwa wanajikinga. Kisha, Yesu alipokuwa na miaka miwili, Mfalme Herode kwa wivu alitaka kumwondoa. Yusufu na Maria walilazimika kukimbilia Misri ili kuepuka dhuluma za Mfalme Herode muuaji.

Nasi tunayo mengi ya kujifunza kutoka kwa Maria tunaposherehekea kuzaliwa kwake, usisingizie wala kukasirika wakati mambo hayaendi kama unavyotaka, mfano  wakati ndoa inaporomoka, kupoteza kazi, kushindwa kufaulu mtihani  pale unapokuwa na matatizo ya kifedha.Lakini usikubali tu hali yako, bali fanya kitu cha kuiokoa. Yesu aliwahurumia wale waliokuwa wagonjwa kwa homa, kudondoka, upofu, viwete, na aliwaponya. Tunapokutana na dhiki kubwa, tufikirie kumwendea Bwana.

Maisha yanapokwenda vizuri, kumbuka kumshukuru Bwana. Hata hivyo, unapokutana na changamoto, kumbuka kwamba Yesu, Maria, na Yusufu walipitia hali mbaya zaidi.

 

Post a Comment

0 Comments