Machapisho yanayopendwa

6/recent/ticker-posts

NINI MAANA YA TOHARANI?


Imani  yetu katoliki inafundisha kuwa Toharani ni sehemu ya mateso, ambapo haki ya Mungu ulipwa.Ni toharani sio mbinguni ambapo kitu chenye uchafu kinaweza   kuingia, sio motoni ambapo hakuna wokovu tena. Toharani ni sehemu ya katikati iliyopo  kati ya furaha  ya milele na mateso yasiyo na mwisho.  Toharani hufanana moto wa milele kwa mateso yake; hufanana mbingu kwa sababu ya utakatifu wa Roho zilizoko huko.

Toharani ni moto unaounguza lakini unasafisha, ni sehemu ya machozi, wakati usafishwaji unapokamilika, Mungu anawaita karibu yake Roho zilizookolewa kwa mateso  anaziunganisha pamoja na furaha yake.

Toharani ni adhabu ya mda na haitakuwepo baada ya hukumu ya mwisho. Hii ndiyo toharani  ni sehemu  ambapo baadhi ya Roho za watu waliokufa bado zinateseka kwa     sababu kwenda moja kwa moja mbinguni ni bahati iliyopo kwa watu wachache sana.

Baadhi ya marafiki zetu wanaweza bado kuwa wako huko. Huko ndipo siku moja tutakwenda itakuwa hivi punde tu. Ni muhimu sana kusali kwa ajili ya Roho ili kwamba nasi      tutakapokuwa  huko waweze kutuombea.

Huko, Roho zinaosha dhambi zao zote. Toharani inahitajika ili         kukamilisha toba, ambayo hatukuimalizia wakati bado  tupo hapa duniani.

Post a Comment

0 Comments