Maneno ya Mwokozi: “Leo niletee
mapadri wote na watawa. Uwazamishe katika kilindi cha huruma yangu isiyo na
mwisho. Ni wao hasa walionipa nguvu ya kuweza kuyavumilia mateso yangu makali
mno. Kwa njia yao, kama vile mifereji, huruma yangu humiminika na kuwatiririkia
wote.”
Tuwaombee mapdri na watawa wote wanawake ili wadumu kiaminifu
katika utumishi wao na wakfu wa maisha yao kwa Yesu Kristu Bwana harusi wao.
Ee Yesu mwenye huruma tele, kwako hutoka
mema yote. Uwazidishie neema yako watawa wanawake waliojitolea na kuwekwa wakfu
katika utumishi wako, ili watekeleze utumishi wao kwa huruma na kwa jinsi
inayofaa, na kwamba wale wanaowaona na kuzishuhudia kazi zao bora, waweze
kumtukuza Baba wa Huruma aliye mbinguni. Amina.
Baba yetu … Salamu Maria … Atukuzwe …
Baba wa Milele, elekeza macho yako yenye huruma, juu ya jeshi teule la wafanyakazi
shambani mwako. Uzitazame kwa wema roho zao mapadre na watawa wote. Uwajalie
wingi wa Baraka zako. Kwa njia ya upendo wa Moyo wa Mwanao, humo ambamo
wameingizwa, uwape nguvu na mwanga, ili waweze kuwaongoza wengine katika njia
ya wokovu, na kwa sauti moja, waihimidi huruma yako kwa nyimbo za sifa bila
mwisho. Amina.
0 Comments