Kwa
ajili ya kuwa Mama wa mkombozi Maria alitajirishwa na Mungu kwa Karama nyingi
zenye kulingana na kazi hiyo kubwa ya kumzaa mkombozi wa Ulimwengu.
Karne kwa
karne kanisa limetambua kwamba Maria aliyejazwa neema na Mungu, alikombolewa
tangu mwanzo kwa kuchukuliwa kwake mimba.
Ndicho yanachofundisha mafundisho ya Imani juu ya kukingiwa dhambi ya asili
yaliyotangazwa na Papa Pius IX alipokiri kuwa fundisho hili la kukingiwa dhambi
ya asili kuwa ni Dogma katika Waraka wake uitwao Ineffabilis Deus,
uliotolewa 8 Desemba mwaka 1854 alisema:
“Mwenye
heri kabisa Bikira Maria, tangu nukta ya kutungwa kwake mimba, kwa neema ya
upendeleo wa pekee wa Mungu mwenyezi, kwa kutazamia mastahili ya Yesu Kristo,
mwokozi wa Wanadamu wote, alikingiwa na kila doa la dhambi ya asili”.
Bikira
Maria kama wanadamu wengine alihitaji kukombolewa dhidi ya dhambi, naye alikombolewa dhidi ya dhambi kwa kutazamia mastahili ya mwanae, kama anavyokiri yeye mwenyewe katika utenzi wake
kwa kusema “Roho yangu imemfurahia Mungu, Mwokozi wangu” Luka 1:47.
Kila mwanadamu isipokuwa Bikira Maria wote alikombolewa
kutoka katika dhambi na upotevu wa milele kupitia mateso na kifo cha Yesu msalabani.
Lakini Mama Bikira Maria yeye alikingwa kabisa dhidi ya dhambi, na dhidi ya
kutenda dhambi.
Ili kuelewa
tofauti ya aina hizi mbili za ukombozi dhidi ya dhambi, fikiria mfano umepigwa
risasi na akaja mtu akakusaidia kuondoa risasi ile na kuponya Donda lako, hakika
utamuita mtu huyo mkombozi wako. Pia fikiria iwapo wakati unataka kupigwa
risasi kabla ya risasi hiyo haijakufikia akaja mtu akakuepusha dhidi ya risasi
hiyo. Hawa wote utawaita wakombozi wako lakini kwa namna tofauti. Wa kwanza
amekukomboa baada ya kupigwa risasi na wapili ni kabla ya kupigwa risasi. Hivi ndivyo
ilivyo hata katika ukombozi wetu na ule wa Bikira Maria.
Zaidi ya
mtu yeyote yule aliyeumbwa, Mungu Baba alimbariki Bikira Maria kwa baraka zote
za Rohoni, katika ulimwengu wa Roho, ndani yake Kristo na akamchagua katika
yeye kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, ili awe mtakatifu na bila
hatia mbele zake katika pendo ili astahili
kumbeba mwanae wa pekee yaani Yesu Kristo, aliyemtakatifu sana, Mungu Baba
asingeweza kuruhusu mwanae akae sehemu yenye dhambi. Kwa neema ya Mungu Mama Maria
amebaki safi kabisa na hakutenda dhambi yoyote Maisha yake yote.
0 Comments