Machapisho yanayopendwa

6/recent/ticker-posts

KWANINI TUNAMUITA MARIA, MAMA WA MUNGU?




Jina la Maria, MAMA WA MUNGU, ni mojawapo ya majina ya zamani na yanayotumiwa mara kwa mara kwa Maria, wakristo wamekuwa wakiitumia  jina ili tangu karne za mwanzo za kanisa. Na hali hii Ya kuwa Mama wa Mungu inafahamika sana hasa kwa jina la kigiriki “Theotokos”. Wakristu wa kwanza walimuita  Maria, Mama wa Mungu bila kusita, kulikuwa na mfano wa maandiko na maandiko hayo yalionekana kuwa na mantiki. Ikiwa Yesu alikuwa Mungu, na Maria alikuwa mama yake, basi hilo lilimfanya awe Mama wa Mungu.

Katika karne ya tano hata hivyo, baadhi  ya wakristu walileta pingamizi sawa na pingamizi linaloonekana kuwepo mpaka leo kwa wasio wakatoliki, walidai kwamba jina MAMA WA MUNGU lilimaanisha kwamba Maria alikuwa “chanzo cha Mungu”. Wapingaji  hao walisema wanaweza kukubali jina “Mama wa Kristu” lakini sio “Mama wa Mungu”.  Walidai Maria alizaa tu asili ya kibinadamu ya Kristo, sio asili ya kimungu ya Kristo.. Kanisa likiongozwa na Papa Celestine I na Mtakatifu Cyril wa Alexandria, lilipinga. Kama vile Mt. Cyril alivyosema “Mama anazaa mtu, sio asili”. Kulingana na  hivyo, Maria alizaa Yesu Kristu, ambaye alikuwa na ni nafsi ya kimungu. Ingawa Maria hakumleta Mungu mwanzo au kumzalisha, lakini alimchukua tumboni mwake na kumzaa, alikuwa MAMA WA MUNGU.

Mgogoro kuhusu cheo cha Maria kama Mama wa Mungu, ulishughulikiwa mwaka 431 B.K, katika Mtaguso wa Efeso. Katika mtaguso  huo kulikuwa na mambo mengi zaidi ya kuongelea kuliko kutetea tu cheo cha Maria, suala kuu lilikuwa fundisho la kikristo kuhusu asili mbili za kristu. Kanisa lilikuwa  na lengo la kutatua swali moja. Je, Yesu alikuwa mtu mmoja au wawili? Kwa kukataa fundisho la mzushi Nestorius, kanisa lilikiri  kwamba Yesu ni mtu mmoja wa kimungu, mwenye asili mbili – asili yake ya kibinadamu kutoka kwa mama yake na asili yake ya kimungu kutoka kwa Mungu Baba.

Maria hakumpa  Yesu asili yake ya kimungu au utu wake wa kimungu – mambo ambayo alikuwa nayo milele kama mwana wa pekee wa Baba. Maria alimzaa Yesu kama mtu mzima alimzaa Yesu Kristo akiwa na asili ya kimungu na ya kibinadamu. Hicho ndicho tunachokiri kila mara tunaposali Kanuni ya Imani.

Kumuita Maria Mama wa Mungu kunathibitisha ukweli ambao lazima usemwe ili kulinda ukweli muhimu kuhusu Kristo. Maria ni kiungo kati ya utu na Umungu wa mwana wake. Yeye ni ishara  kwamba Yesu ni Mungu-Mtu.


Post a Comment

0 Comments