Machapisho yanayopendwa

6/recent/ticker-posts

KUPALIZWA BIKIRA MARIA MBINGUNI


Dogma ya Kupalizwa Mbinguni inafundisha kwamba mwishoni mwa maisha yake duniani, Maria alichukuliwa—mwili na roho—kwenda mbinguni. Huko, anaketi upande wa kulia wa Mwana wake, akiwa Mfalme wa Mbinguni na Duniani. Misingi ya mafundisho haya inatokana na Maandiko. Kupalizwa Mbinguni  ilitagazwa kama dogma iliyoelezwa ya Kanisa Katoliki mnamo 1950 na Papa Pius XII aliposema "Kwa mamlaka ya Bwana wetu Yesu Kristo, ya Mitume Watakatifu Petro na Paulo, na kwa mamlaka yetu wenyewe, sisi tunatangaza, na kuidhinisha kuwa ni dogma iliyofunuliwa kimungu: kwamba Mama Mtakatifu wa Mungu, Bikira Maria, akiisha kumaliza safari ya Maisha yake duniani, alichukuliwa mwili na roho katika utukufu wa mbinguni."

Katika chapisho langu juu ya kukingiwa kwake Bikira Maria dhidi ya dhambi, Nimeeleza kuwa Krsto alimheshimu mama yake kwa kumlinda dhidi ya  dhambi tangu mwanzo wa maisha yake. Hiyo ingekuwa heshima ya kutosha, lakini tunajua kwamba hakuishia  hapo. Kama alivyopokea ukombozi kama matunda ya kwanza ya kazi ya Kristo, vivyo hivyo alipokea ufufuo wa mwili na utukufu wa mbinguni.

Ushahidi wa maandiko juu ya kupalizwa kwake mbinguni unaweza kufuatiliwa hadi karne ya nne. Kufikia mwishoni mwa karne ya sita, mafundisho na sikukuu yalikuwa tayari yamekubalika kote Kanisani. Hakuna ushahidi wa kutosha kwamba mafundisho hayo yalipingwa au kuhojiwa kwa dhati wakati huo wa Kanisa; wala kanisa wala jiji lolote halijawahi kudai umiliki wa mabaki ya Bikira Maria. Hilo, peke yake, ni jambo la kuvutia. Kanisa la mapema, miji, na makanisa vilishindania mabaki ya mitume wakuu na mashahidi. Kama mabaki ya Maria yangelikuwa duniani, yangelikuwa zawadi kubwa, na utafutaji na uhamishaji wa mabaki hayo kutoka jiji hadi jiji ungekuwa na ushuhuda mzuri. Lakini tena, rekodi ya kihistoria haionyeshi dalili hata moja ya kisanduku cha mabaki ya Maria—isipokuwa kaburi lake tupu. (Na miji miwili inadai zawadi hiyo!).

Tunapata taarifa ya tukio hilo kidogo zaidi iliyotulia kutoka kwa Mtakatifu Yohane wa Damasko katika nakala ya barua aliyoihifadhi kutoka kwa Kiongozi mkuu wa Yerusalemu wa karne ya 5 anayeitwa Juvenalius kwa Malkia Mzuri wa Byzantine Pulcheria. Inaonekana Malkia alikuwa ameomba masalia ya Mama Mtakatifu Bikira Maria. Juvenalius alijibu kwamba, kulingana na mapokeo ya zamani, mwili wa Mama wa Mungu ulichukuliwa mbinguni baada ya kifo chake, na akastaajabu kwamba Malkia hakuwa akiifahamu hii (akimaanisha kwamba ilibidi iwe maarufu katika Kanisa wakati huo).

Juvenalius aliambatanisha barua hii na taarifa ya jinsi mitume walivyoitwa kwa njia ya miujiza kwa mazishi ya Mama wa Mungu, na jinsi baada ya kufika kwa mtume Tomaso, kaburi lake lilifunguliwa, na mwili wake haukuwepo, na jinsi ilifunuliwa kwa mitume kwamba alikuwa amechukuliwa mbinguni, mwili na roho. Baadaye, karne ya 6, fundisho juu ya kupalizwa mbinguni lililindwa na Mtakatifu Gregori wa Tours, na hakuna mtakatifu au mwanafalsafa wa Kanisa aliyepinga imani hiyo baadaye.

Ni dhahiri, vipande hivi vya ushahidi pekee havithibitishi kwamba mafundisho haya ni kweli. Lakini Kanisa linaamini kwamba kutokana na kumwagika kwa Roho Mtakatifu katika Pentekoste, watu wa Mungu kwa ujumla wanayo ile ambayo Mtakatifu Agustino na Mtakatifu Tomaso wa Aquino waliiita affectio au inclinatio fidei. Yaani, mwelekeo wa kihisia unaowavuta kwa ukweli wa imani. Kwa kuwa Roho Mtakatifu ni Roho wa Kweli, makubaliano ya waamini kuhusu jambo la kweli la kiungu, na haswa ya watakatifu (ambao wamejaa Roho Mtakatifu), hakika si jambo la kupuuzwa.



Pili, inadaiwa kwamba hakuna maelezo ya kupalizwa kwake Bikira  Maria katika Maandiko. Lakini ningedai (nikimfuata msomi na mwalimu wa Kikatoliki anayeitwa Scott Hahn) kwamba kuna, mrejeo wa mafumbo ya kupalizwa moja kwa moja katika sehemu tunayotarajia kuipata ikiwa mafundisho yalikuwa kweli: yaani, katika maandishi ya Mtume Yohane, yule ambaye Bwana alimkabidhi Mama yake saa ya kifo chake Msalabani, na haswa katika kitabu ambacho labda ni cha mwisho katika Agano Jipya kuandikwa, kitabu cha Ufunuo.

Katika kitabu chake kipya, kinachoitwa Hail Holy Queen, Profesa Hahn anaonyesha kwa hakika kwamba hadithi ya Bikira Maria kumtembelea  binamu yake Elizabeti katika Injili ya Luka, sura ya kwanza, ina fanano nyingi na ya kushangaza na  ya Agano la Kale ya Mfalme Daudi kuletewa Sanduku la Agano hadi Yerusalemu katika 2Samweli 6.

Mfanano huu haukuwa wa bahati mbaya: Yohane wa Damasko anatuambia, kwa njia yake ya kipekee, kwamba Maria mwenyewe ni Sanduku jipya la Agano. Kama vile Sanduku katika Israeli ya zamani lilikuwa na mbao za Amri za Mungu na baadhi ya mana ya mkate kutoka mbinguni - ishara za Agano la Kale - hivyo tumbo la Maria lilikuwa na ishara ya ahadi ya Agano Jipya na Mkate wa Kweli wa Uzima: Yesu Mwokozi wetu Mwenyewe. Hivyo, ilikuwa tayari imani ya Kanisa la Mitume kwamba Maria alikuwa Sanduku jipya la Agano.Sasa, Sanduku la Kale la Agano lilipotea kwa karne nyingi, na Wayahudi wengi hawakujua mahali ambapo wangeweza kulipata (kwa kweli, bado linaonekana kupotea mpaka leo).

 


Ikiwa tunazingatia hili, sasa tutizame tunachokipata kwa kusoma  mwishoni mwa sura ya 11 ya Kitabu cha Ufunuo:

“Ndipo hekalu la Mungu mbinguni likafunguliwa, na sanduku la agano lake likaonekana ndani ya hekalu lake, kulikuwa na umeme, sauti, ngurumo, tetemeko la ardhi na mvua kubwa”.

Wow, ni onyesho la sauti na la kuonekana! Sanduku lilikuwa limepatikana! Lakini tunapoangalia kitabu cha Ufunuo kinatuambia baadaye (na kumbuka: sehemu na sura za Biblia si sehemu ya maandishi ya awali: ziliwekwa na wamonaki muda mrefu baadaye ili kutusaidia kuona mistari ya Maandiko kwa urahisi zaidi, kwa hivyo sentensi ifuatayo mwanzoni mwa sura ya 12 ilifuata moja kwa moja ile mwishoni mwa sura ya 11 katika maandishi ya awali):

“Na alama kubwa ikatokea mbinguni, mwanamke amevikwa jua, na mwezi chini ya miguu yake, na juu ya kichwa chake taji ya nyota kumi na mbili; alikuwa mjamzito... [alimzaa mtoto wa kiume, yule atakayewachunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma]”.

Dhahiri, kile ambacho Yohane alionyeshwa katika maono yake, kilichorekodiwa hapa katika Kitabu cha Ufunuo, ni kwamba Sanduku la Agano sasa liko mbinguni kama "mwanamke amevikwa jua" ambaye mwana wake ni Masihi (atakayetawala kwa "fimbo ya chuma," kulingana na Zaburi 2:9).

Hakika, baadhi ya mababa wa Kanisa waliona kifungu hiki kama marejeo kwa Maria, Mama wa Mwokozi wetu, ikiwa ni pamoja na Mtakatifu Ephrem, Mtakatifu Ambrose, na Mtakatifu Agustino. Wakati huo huo, wengi wa Mababa waliona "mwanamke" anayetajwa kama ishara ya Israeli, na Kanisa, Israeli Mpya. Kuna hakika ishara kwamba hii pia ndio inayoonesha na ishara hapa (kwa mfano, ana taji ya nyota kumi na mbili kichwani mwake, ikionesha kabila kumi na mbili za Israeli, na mitume kumi na mbili).

Kwa hivyo ni tafsiri ipi sahihi? Zote mbili ni sahihi! (Na Mababa wa zamani hawakuona mgongano kati yao.) Haikuwa nadra katika fasihi ya Kiyahudi ya zamani kutumia mfano wa mara mbili: mtu halisi kutumika kama ishara ya kikundi kizima cha watu. Kwa mfano, ni kwa kiasi kikubwa kwamba kifungu maarufu katika Isaya 53 kuhusu mateso ya Masihi ("Alikuwa mwenye dhihaka na kupuuzwa na watu, mtu wa huzuni na kujua mateso," n.k.) pia ni ishara ya wito wa mateso wa watu wote wa Israeli. 

Kwa njia sawa, Maria, Mama wa Kanisa, inatumiwa katika kitabu cha Ufunuo kuwakilisha utimilifu wa wito wa Israeli katika watu wa Mungu wapya, ambao watabeba Kristo ulimwenguni. Si ajabu kwamba Kanisa lilipoanza kuandaa maandishi ya liturujia kwa Sikukuu ya Kupalizwa Mbinguni, lilifanya uhusiano (ulioanzishwa awali na baadhi ya Mababa wa zamani), kati ya Zaburi 131:8 na siri ya mwanamke ambaye ni sanduku la mbinguni: "Simama, Bwana, ingia mahali pako pa raha, Wewe na sanduku la nguvu zako." Baada ya Bwana "kuinuka" kutoka kwa wafu, Alikwenda naye mbinguni pamoja na "sanduku" halisi la Agano Jipya, mwili wa Mama yake Maria. Kwa kuwa Wayahudi wa kale waliamini kwamba sanduku la asili lilifanywa kwa mbao isiyoharibika, hivyo kifungu hiki kinatabiri kifo kisichoharibika alichopewa Maria na Mwana wake aliyefufuka.  Kristo alileta sanduku la agano jipya yaani Bikira Maria kuishi katika patakatifu  ndani ya hekalu la Yerusalemu ya mbinguni.

Hatimaye, naamini   Kupalizwa kwake  Mbinguni Bikira Maria ni ukumbusho wa ukweli wa kufufuka. Tunapata muono wa zawadi iliyoahidiwa na kifo na ufufuko wa Bwana Yesu. Kama vile Yesu anavyosema katika Injili ya Yohane, "Katika nyumba ya Baba yangu mna makao mengi. Naenda kuwaandalia mahali." Mama wa Yesu amekwenda kwenye nyumba ya mbinguni. Lakini Maria ni Mama yetu pia! Je, usingefikiri kwamba pale Mama yetu alipo, huko ndiko tutakakokuwa?

 

Post a Comment

0 Comments