Mafundisho ya ubikira wa daima wa Maria ni mojawapo ya mafundisho yenye muda mrefu zaidi katika Kanisa. Mafundisho haya yalifundishwa na Mababa wa Kanisa wa mwanzo, ikiwa ni pamoja na: Tertullian, Mt. Athanasius, Mt. Ambrose, na Mt. Augustine. Na ilitangazwa rasmi kuwa dogma kwenye Baraza la Ekumeni la Tano huko Konstantinople mnamo mwaka 553 B.K. Tangazo hilo lilimuita Maria "daima bikira." Karne moja baadaye, taarifa ya Papa Martin I ilifafanua kwamba "daima bikira" inamaanisha kwamba Maria alikuwa bikira kabla, wakati, na baada ya kuzaliwa kwa Kristo.
Kati ya
aina hizo tatu za ubikira wa daima wa Maria, sehemu
rahisi zaidi kuona katika Maandiko ni mimba yake ya bikira kwa Kristo. Mathayo
na Luka wanaelezea kuhusu hilo rejea Mt 1:18; Lk 1:34–35, 3:23.
Uzazi huo wa bikira ni dhamana ya umungu na ubinadamu wa Yesu. Inalinda ukweli
kwamba yeye alikuwa Mungu kamili na mwanadamu kamili.
Kidogo
kinachoonekana ni ngumu kueleweka ni ubikira wa Maria wakati na baada ya kuzaliwa kwa Kristo.
Kuelewa sababu ya hilo kunahitaji kutambua kwamba ubikira wa Maria haukuwa tu
sifa mojawapo kati ya nyingine. Ni kitovu cha utambulisho wake. Maisha yake
yote, Maria alikuwa na ukamilifu ambao kila binadamu tangu Adamu na Hawa
amekosa. Kwa sababu ya ukamilifu huo, mwili wake ulielezea kikamilifu roho
yake. Hakukuwa na mvutano kati ya hivyo viwili. Kulingana na hilo, kwa kuwa
roho ya Maria ilikuwa imetolewa kabisa kwa Mungu, vivyo hivyo ilikuwa mwili
wake. Ubikira wake wa mwili ulikuwa ni ishara endelevu ya utakatifu huo.
Ubikira
wa Maria unahifadhi ishara ya kimwili ya ukweli wa ndani. Kufanya hivyo
kulihitaji muujiza, lakini si zaidi ya muujiza uliotokea kwa Yesu, baada ya
kufufuka kwake, kuingia kwenye chumba ambapo wanafunzi wake walikuwa
wanamngojea ingawa mlango ulikuwa umefungwa (Yoh 20:19). Hii ni mojawapo ya
sababu pia kwa nini Maria na Yosefu walijizuia kutoka kwa uhusiano wa kawaida
wa ndoa. Ubikira wake ulikuwa muhimu mno kwa utambulisho wake.
Mafundisho haya juu ya Ubikira wa Maria,
yanatabiriwa
katika "aina" mbili za Agano la Kale: Bikira na Sanduku la Agano.
Utakatifu wa Sanduku ulitokana na uwepo wa Mungu ndani yake. Uwepo huo ulifanya
kuwa takatifu hivi kwamba mtu yeyote aliyekigusa alikufa papo hapo (2 Samweli
6:6–7). Maria, kama Sanduku, alikuwa ameitwa mbali na vitu vyote vingine katika
uumbaji. Alikuwa na uwepo wa Mungu ndani yake, uliofungwa kwa kila mtu na kila
kitu kingine katika heshima hii.
0 Comments