Machapisho yanayopendwa

6/recent/ticker-posts

NOVENA YA HURUMA YA MUNGU SIKU YA NANE


 

Maneno ya Mwokozi: “Leo niletee roho za wale waliofungwa bado toharani, na uwazamishe ndani ya Bahari Kuu ya Huruma yangu. Humo, mafuriko ya Damu yangu, yazimishe miali ya motto mkubwa unaowachoma. Roho hizi zote hupendwa sana nami.  Wako humo toharani kwa ajili ya kulipia Haki yangu waliyoikosa hapa duniani. Wewe una uwezo wa kuwapatia faraja. Chota rehema zote za Kanisa langu na uzitolee kwa ajili yao. Ungalijua tu ukali wa mateso yao, loo! Ungetolea daima sadaka za kiroho kwa ajili yao, na kulipa deni zima la Haki ya Mungu”.

Tuwaombee marehemu wa toharani, wanaoilipia Haki ya Mungu, ili mtiririko wa Huruma wa Damu ya Yesu uweze kupunguza na kufupisha mateso yao.

Ee Yesu mwenye Huruma uliyesema, “Muwe na Huruma kama Baba yenu wa mbinguni alivyo na Huruma”. Uzitazame kwa Huruma roho zile zinazoteswa toharani, kwa kulipia deni la Haki ya Mungu waliyoikosea. Mtiririko ule wa Damu na Maji uliotoka kwa kasi Moyoni mwako, uzimishe miale ya moto mkali wa toharani, ili huko pia Huruma yako isifiwe na kuadhimishwa. Amina.

Baba yetu … Salamu Maria … Atukuzwe …

Baba wa Milele, uzitazame kwa wema na huruma, roho zile zinazoteswa Toharani, wao pia wameingizwa ndani ya Moyo wa Mwanao Mpenzi Yesu, na uchungu wote ulioelemea Moyo na Roho yake, onyesha Huruma yako kwa roho zilizotiwa nguvuni na Haki yako. Uwatazame watu hao kwa njia ya Madonda yake Yesu Mwanao Mpenzi, kwa kuwa tunaamini kabisa kuwa wema na Huruma yako havina mwisho. Amina

Post a Comment

0 Comments