Maneno
ya Mwokozi: “Leo niletee roho za wale waliokwishaingia hali ya uvuguvugu, na
uwazamishe katika kilindi cha Huruma yangu. Roho hizi huumiza sana Moyo wangu.
Roho yangu iliteseka sana kwa kinyaa cha kutisha kule bustanini kwa sababu ya
roho hizi vuguvugu. Ni wao waliosababisha nilie; Baba ikiwa ni mapenzi yako
uniondolee mbali kikombe hiki nisikinywe. Kwa watu hawa, tumaini la mwisho
lililowabakia ni kuikimbilia Huruma yangu tu basi”.
Kiongozi:
Tuwaombee watu walio na hali ya uvuguvugu, hali ya hatari kwa wokovu, ambao
walisababisha mateso makali sana kwa Yesu Kristu kule bustanini mwa mizeituni.
Ee
Yesu mwenye Huruma nyingi, Wewe u Huruma yenyewe, Uzipokee roho vuguvugu ndani
ya Moyo wako ulio na Huruma bila kiasi. Roho hizi ni kama mizoga iliyojaa na
kunuka uvundo, uziingize katika moto wa upendo wako safi, zitakasike. Roho hizi
zilikutia kinyaa kingi. Sasa uziwashe tena, na kwa Huruma yako, uzipe paji la
Upendo Mtakatifu. Ee Yesu mwenye Huruma Kuu, tumia uwezo wako na uzipatie roho
hizi bidii tena, kwani kwako hakuna kitu kisichowezekana, na kwa njia hii
wapate kuitukuza daima Huruma Yako. Amina
Baba
yetu... Salamu Maria … Atukuzwe...
Baba
wa Huruma, uzitazame kwa macho ya Huruma, roho zilizo vuguvugu, ambazo katika
hali yao hiyo, wameingizwa ndani ya Moyo wa Mwanao Yesu, ulio kilindi cha
Huruma. Ee Baba wa Huruma, tunakusihi kwa ajili ya mateso makali ya Mwanao
Mpenzi, Bwana wetu Yesu Kristu, uliyovumilia pale msalabani, kwa masaa matatu
ukiwa katika hali ya umahututi ya uchungu, uziwezeshe hata roho hizi zipupie
utukufu wako. Uijaze mioyo ya watu hawa upendo wa kweli, hivyo kwa Baraka
takatifu, waweze kutenda matendo mengi ya huruma hapa duniani, na huko Mbinguni
wafike kuitukuza Huruma yako Kuu kwa milele yote. Amina
0 Comments