Rozari hii ilitolewa na Yesu mwenyewe kwa sista
Faustina huko Vilnius tarehe 13-14. Septemba 1935 kama sala ya malipizi ya
dhambi zetu.
Mtakatifu Faustina alipata maono ya Malaika wa Bwana
aliyetumwa kuangamiza mji Fulani. Sista Faustina alianza kuomba huruma lakini
sala zake hazikuwa na nguvu yoyote. Ghafla hakaona Utatu Mtakatifu na nguvu ya
neema ikamjia. Wakati huo alijikuta anamuomba Mungu huruma yake kwa maneno
aliyoyasikia ndani ya moyo wake “Baba wa milele ninakutolea Mwili na damu,
Roho na Umungu wa Mwanao mpenzi, bwana wetu Yesu Kristo, kwa kulipia dhambi
zetu na dhambi za dunia nzima, kwa ajili ya mateso makali sana ya Yesu
utuhurumie sisi na dunia nzima” Alipokuwa akiendelea kusali sala hii,
Malaika alionekana kushindwa kutimiza adhabu hiyo (Shajara, 474,475 na 476).
Asubuhi ya siku iliyofuata aliingia kanisani alisikia tena moyoni mwake
sauti ikisema hivi; “kila mara unapoingia kanisani Sali sala
niliyokufundisha jana.. sala hii itatuliza adhabu yangu. Utaisali kwa siku tisa
katika punje za rozari kama ifuatavyo : kwanza utasali BABA YETU na SALAMU
MARIA na KANUNI YA IMANI. Kisha katika punje za Baba Yetu utasema maneno
yafuatayo “ “Baba wa milele ninakutolea Mwili na damu, Roho na Umungu wa Mwanao
mpenzi, Bwana wetu Yesu Kristo” na kwenye punje za Salamu Maria utasema maneno
yafuatayo; “kwa ajili ya mateso makali sana ya Yesu utuhurumie sisi na dunia
nzima”. Kwa kuhitimisha utasali mara tatu; “ Mungu Mtakatifu, mtakatifu mwenye
enzi, mtakatifu usiyeweza kufa, utuhurumie sisi na dunia nzima”.
Tangu siku hiyo aliendelea kusali sala hiyo bila
kukoma, akitoa hasa kwa ajili ya wanaokufa. Katika mafunuo mengine, Yesu
alimdhihirishia kuwa Rozari hiyo haikuwa yake hasa, bali ilikusudiwa kwa ajili
ya dunia nzima. Alitoa pia ahadi zisizo za kawaida kwa wale watakaoisali: “uwatie
watu moyo ili wasali rozari hii niliyokupatia”. (shajara 1541) “yeyote
akayeisali atapata huruma kuu saa ya kufa”(shajara 687) “watakaposali Rozari
hii mbele ya mtu anayekufa, nitasimama kati ya Baba yangu na mtu huyo, si kama
hakimu mwenye haki, bali kama MWOKOZI mwenye huruma” (shajara 1541). “ mapadre
wawatolee wadhambi sala hii kama matumaini yao ya mwisho na wawafundishe hivyo.
Hata mtu angekuwa na dhambi nyingiau Roho ngumu kiasi gani, asalipo rozari hii
hata mara moja tu, atapata neema zangu zisizo
na mipaka”(shajara 687). “rozari hii itakupatia kila kitu, iwapo maombi yako
hayatapingana na mapenzi yangu”. (Shajara 1731).
Rozari hii inaposaliwa kwa kutumia Rozari ya kawaida,
Rozari ya huruma ya Mungu ni sala ya maombezi yenye nguvu ya kuongeza ukuu wa
sadaka ya Ekaristi, hivyo inafaa isaliwe
baada ya mtu kuwa amepokea komunyo takatifu kwenye Misa takatifu. Inaweza
kusaliwa muda wowote, lakini Bwana wetu alimwambia mtakatifu Sista
Faustina kuisali siku tisa kabla ya
Sikukuu ya Huruma ya Mungu. Na alisema; “ kwa novena hii nitazipatia Roho neem
azote zinazowezekana” (Shajara, 796).
Wataalamu wengi wa teolojia na ujumbe wa huruma ya
Mungu wanasema mwamini anayesali kwa uchaji Rozari ya huruma anatimiza ukuhani
wa Mkristo utokanao na ubatizo wake na kimsingi anatenda yale atendayo kuhani
altareni anapogeuza mkate na divai kuwa
mwili wa bwana na damu yake ya thamani. Si kwamba, mkristo ana uwezo wa kutenda
mageuzo kama padre wakati wa misa, lakini kwa kusali rozari ya huruma anatimiza kikamilifu Ukuhani wake
utokanao na ubatizo wake na kumtolea Mungu mwenye huruma sadaka ya Bwana wetu Yesu
Kristo aliyoitoa msalabani siku ya ijumaa kuu.
x
0 Comments