Machapisho yanayopendwa

6/recent/ticker-posts

NOVENA YA HURUMA YA MUNGU SIKU YA NNE

 



Maneno ya Bwana Yesu: “Leo niletee wale wote wasioniamini na wale wasionijua bado. Wao pia niliwafikiria wakati wa mateso yangu makali, na juhudi watakayokuwa nayo baadaye ilinituliza Moyo wangu. Uwaingize katika Bahari Kuu ya Huruma Yangu.”

Tuwaombee watu wote wasiomwamini Kristu, pamoja na wale wasiomjua bado.

Ee Yesu mwema, Wewe ni Mwanga wa dunia nzima, uzipokee katika makao ya Moyo wako wenye huruma sana, roho za wale wote wasiokuamini na wale wasiokujua bado. Achia mionzi ya neema yako iwaangazie, ili nao pia pamoja nasi sote. Waweze kuitukuza huruma yako ya ajabu, na usiwaache wakatoroka makao hayo, ambayo ni Moyo wako uliojaa huruma. Amina.

 Baba yetu … Salamu Maria … Atukuzwe …

Baba wa Milele, elekeza macho yako yenye huruma, kwa roho za watu wale wasiomwamini Mwanao, na za wale ambao hawajakujua Wewe bado, ambao tumewaingiza ndani ya Moyo wa Yesu uliojaa huruma tele. Uwavute kwenye mwanga wa Injili, watu hawa hawajui Ukuu wa furaha iliyopo katika kukupenda Wewe. Uwajalie nao pia waweze kuitukuza hisani ya huruma yako, kwa miaka isiyo na mwisho. Amin

Post a Comment

0 Comments