Machapisho yanayopendwa

6/recent/ticker-posts

MFAHAMU MTAKATIFU SISTA MARIA FAUSTINA KOWALSKA

 


Mtakatifu Maria Faustina Kowalska, anafahamika leo kama “Mtume wa Huruma ya Mungu”.

Alizaliwa kama mtoto wa tatu katika familia ya Watoto kumi, familia yake ilikuwa maskini na waliishi huko katika Kijiji cha Glogowiec, kilichopo nchini Polandi. Alibatizwa katika kanisa la  Parokia ya karibu iliyokuwa Swinice na alipewa jina la “Helena”.  Tangu alipokuwa mdogo alikuwa tofauti na wenzake kwani alikuwa ni mcha Mungu, alipenda sala, mwenye kujituma na mtii, aidha alikuwa ni mwenye huruma sana kwa watu waliokuwa wakiteseka na taabu mbalimbali. Alisoma kwa muda wa miaka mitatu, na alipofikisha umri wa miaka kumi nne kutokana na hali duni ya familia yao aliondoka katika makazi ya familia yao na kuamua kutafuta kazi ili kusaidia familia yake, na alifanya kazi za ndani katika miji ya karibu na kwao ya Aleksandrow na Lodz.

Alipokuwa na umri wa miaka saba (miaka miwili kabla ya kupokea komunio), Helena tayari alihisi katika Roho yake wito wa kuingia katika Maisha ya kitawa. Alipowaeleza wazazi wake juu ya wito wake huo wazazi wake walimkatalia. Kwa sababu ya kukataliwa alijitahidi kuzuia wito huu wa kimungu uliokuwa ndani yake. Baada ya siku nyingi kupita siku moja alipewa  maono ya Yesu akiwa anateseka na alimsikia Kristu akimwambia “nitaendelea kukaa na wewe mpaka lini na wewe utaendelea kuniacha mpaka lini”,  baada ya maono hayo alianza kutafuta nyumba ya masista(conventi) ambayo angejiunga nao. Alikwenda katika nyumba nyingi za kitawa lakini sehemu zote alikataliwa. Hatimaye tarehe 01.Agosti. 1925, alikubaliwa akaanza kukaa katika nyumba ya watawa wa Bibi yetu wa Huruma iliyokuwa katika mtaa wa Zytnia huko Warsaw. Katika kitabu cha Maisha yake aliandika hivi “ilionekana kwangu kama nimeingia katika Maisha ya Paradiso. Sala moja ilikuwa ikitoka moyoni mwangu nayo ilikuwa sala ya shukrani”.

Baada ya wiki chache kupita alipitia kishwawishi kikubwa cha kutaka kuhama Kwenda katika nyumba ya shirika jingine la kitawa ambapo alitamani kuwa angepata muda mwingi wa kusali. Akiwa katika hali hiyo Bwana wetu alimtokea, alioneshwa uso wa Yesu ulioteswa, na Bwana alimwambia “ni wewe utakaye sababisha maumivu haya kwangu utakapoondoka katika conventi hii. Mimi nimekuita katika conventi hii na sio sehemu nyingine, na katika sehemu hii nimekuandalia neema nyingi sana kwa ajili yako”.

Alipojiunga na masista hao alipewa jina la Sista Maria Faustina. Alifanya unovisi wake huko Cracow,  huko Cracow Askofu Stanslaus Rospond, alimpa nadhiri zake za kwanza, miaka mitano baadae aliweka nadhiri zake za daima za Usafi wa moyo, umaskini na utii. Alipewa kazi katika nyumba zao za kitawa, lakini hasa huko Cracow, Plock na Vilnius, alifanya kazi za kupika, kutunza bustani na kukaa getini.

Kwa mwonekano wake wa nje hakuna kitu chochote kilichoonekana cha ziada. Alifanya kazi zake, alifuata sheria zote za kitawa, alikuwa mtulivu na mwenye kukaa kimya, alikuwa mchangamfu siku zote, alijaa ukarimu na upendo usio wa kibinafsi kwa Jirani.

Maisha yake yote yalihusisha kutafuta ukamilifu wa muungano wa kweli kwa Mungu, kujitoa binafsi katika kushirikiana na Yesu katika kazi ya kuokoa Roho. Katika kitabu cha Maisha yake aliandika “unajua toka mwanzo wangu nimekuwa nikitaka kuwa mtakatifu mkubwa, yani hii inamaanisha nimekuwa nikitaka kukupenda wewe kwa upendo mkubwa ambao hakuna Roho umewahi kukupenda hivyo”.

Ni katika kitabu chake cha “Diary” yaani “Shajara” ambacho kinatufunulia kina cha Maisha yake ya kiroho. Unaposoma kwa makini kitabu cha Maisha yake kinatoa picha ya kilele kikubwa cha umoja uliokuwepo baina ya Roho yake na Mungu, uwepo wa karibu sana wa Mungu kwa Roho yake, Pamoja na jitihada zake na magumu yake katika njia ya kuuutafuta ukamilifu wa kikristo. Bwana alimpa neema kubwa sana neema ya kutafakari, kwa ufahamu wa kina sana mafumbo ya  huruma ya Mungu, kwa maono, ufunuo, madonda yaliyofichika, alipewa zawadi ya unabii na kuelewa Roho za watu.



Maisha magumu na Maisha ya kufunga aliyoakuwa akiishi hata kabla ya kujiunga na shirika lake la kitawa, yaliudhoofisha sana mwili wake kiasi kwamba wakati akiwa mpostulanti alitakiwa apelekwe huko  Skolimow karibu na Warsaw ili kuweka afya yake sawa. Mwishoni mwa mwaka wake wa kwanza wa unovisi, alipatwa na maumivu yasiyo ya kawaida ya ajabu yafahamikayo kama “Usiku wa giza” (Dark night), na baadae alipata mateso kiroho yaliyohusiana na kukamilisha kazi yake aliyokuwa akipewa na Kristo Bwana. Mt. Faustina aliyatoa Maisha yake sadaka kwa ajili ya wadhambi na kwa sababu hii alipitia mateso makubwa sana, ili kuokoa Roho mbalimbali za watu. Miaka yake ya mwisho wa Maisha yake alipitia  mateso ya ndani ya mwilin na Roho yaliongezeka sana. Aliugua ugonjwa wa Kifua kikuu ulioshambulia mapafu yake na mfumo wake wa mmengenyo wa chakula. Kwa sababu hii alipelekwa hospitali kwa miezi kadhaa ili kutibiwa huko katika mtaa wa Pradnik jijini Cracow.

Akiwa amedhoofika sana kimwili lakini amekomaa kiroho alifariki na kuugana na Mungu tarehe 05. Oktoba.1938, akiwa na umri wa miaka 33, na alikuwa mtawa kwa muda wa miaka 13. Mwili wake ulizikwa katikaa makaburi ya watawa huko Cracow-Lagiewniki. Na mwaka 1966, mwili wake uliamishwa wakati wa hatua za kutangazwa kwake mtakatifu na uliwekwa katika kikanisa cha masista.

Kwa mwanamke huyu wa kawaida asiyekuwa msomi, lakini mtawa jasiri,  aliyemwamini bwana wetu bila kikomo, Bwana wetu alimpa kazi kubwa ya kutangaza ujume wake wa Huruma kwa ulimwengu wote, alimwambia “Leo ninakutuma  kwa huruma  kwa watu wa ulimwengu wote. Sitaki kuadhibu wanadamu, lakini ninatamani kuwaponya, kuwaweka katika moyo wangu wa huruma” (Shajara, 1588) “Wewe ni karani wa huruma yangu, nimekuchagua wewe kwa kazi hiyo katika Maisha haya na yale yajayo”(Shajara, 1605).

Post a Comment

0 Comments