Machapisho yanayopendwa

6/recent/ticker-posts

Bikira Maria Katika Mawazo ya Mungu


Kabla ya kupata mwenzi wa kungia nae katika mahusiano nae pengine kuishi pamoja nae katika ndoa takatifu, hakika kila mmoja anakuwa tayari na vigezo au sifa fulani anazotamani kuziona kwa mwenzi wake; mtu anakuwa na yale anayoyapenda na asiyoyapenda, baadhi ya watu watakuwa na sifa hizo na wengine watakosa sifa hizo.

Baba wa milele

Mungu pia wakati wa uumbaji wake tayari alikuwa na namna alivyotaka ulimwengu uonekane, kama ilivyokawaida kabla ya kujenga nyumba mjenzi anahitaji ramani ya nyumba ili kutekeleza ujenzi wa nyumba vizuri. Kila kitu kilichopo duniani hapa kilikuwepo katika akili ya Mungu tangu milele yote.

Mungu alipomuumba mwanadamu alikuwa na mawazo mawili juu ya mwanadamu kwanza ni vile atakavyokuwa mwanadamu yaani umbile lake na pili ni vile atakavyo takiwa kuishi. Lakini mwanadamu hakuweza kuishi vile alivyotakiwa kuishi, aliishi kinyume na mpango wa Mungu juu yake.

Mwanadamu mmoja tu ndiye aliyeishi kwa asilimia mia moja, yaani aliishi kikamilifu kwa kadri ya mpango wa Mungu juu ya kila mwanadamu, mwanadamu huyu si mwingine bali ni Bikira Maria. Mawazo ya Mungu juu ya Maria yalikuwa sawasawa na jinsi Maria alivyoishi hapa duniani.

Kwa kuwa yeye ndiye vile ambavyo Mungu alitaka sisi sote tuwe, Maria ni mfano wa milele akilini mwa Mungu, yule ambaye Mungu alimpenda hata kabla ya kuumbwa kwake. Maria alikuwa pamoja na Mungu si tu wakati wa uumbaji, bali hata kabla ya uumbaji. Yeye alikuwepo katika akili ya Mungu ata kabla ya kuwepo kwa mama yeyote. Yeye ndiye Mama wa Mama wote duniani.

Mungu si tu alimfikiria katika milele yote, bali pia alimfikiria mwanzoni mwa wakati, mwanzo wa historia ya mwanadamu, wakati binadamu walipoanguka kwa kushawishiwa na mwanamke, Mungu alimwambia shetani “Nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na wake, huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino” (Mwanzo 3:15). Mwanamke anayezungumziwa hapa ni Bikira Maria sio Eva, kwa kuwa Eva tayari alikubali kuwa chini ya shetani kumuasi Mungu asingeweza kuwa adui wa shetani. Ni kama Mungu alikuwa akisema ikiwa ni kwa mwanamke wanadamu walianguka, basi ingekuwa kwa njia ya mwanamke ambayo angelipiza kisasi kwa shetani.

maria

Yeyote ambaye angekuwa Mama wa Mungu, bila shaka angebarikiwa kati ya wanadamu wote, na kwa sababu Mungu mwenyewe alimchagua, angehakikisha kuwa vizazi vyote vinamwita mbarikiwa.

Post a Comment

0 Comments