Machapisho yanayopendwa

6/recent/ticker-posts

Ibada ya Salamu Maria Tatu

 

Mama Maria
Ibada kwa Bikira Maria Mtakatifu ni moja kati ya njia kuu za wokovu. Mtakatifu Alphonsus Maria Liguori aiiandika katika moja ya vitabu yake: "Mtumishi mcha Mungu wa Maria hataangamia kamwe." Jambo kuu ni kuendelea kuwa waaminifu hadi kifo katika ibada hii kwa Bikira Maria.

Je, ungependa kumwona Mama Bikira kabla ya kufa? Hapa kuna ibada rahisi ambayo Bikira Maria mwenyewe alimfundisha Mtakatifu Mechtilde  mwaka 1270. Ibada hii inajulikana kama "Ibada ya Salamu Maria Tatu," na inajumuisha kusali Salamu Maria tatu kila siku na kisha kusali kwa kusema "Ewe Mama yangu, unikinge na dhambi ya mauti mchana huu (au usiku)". katika Ibada hii Salamu Maria inasaliwa mara tatu kwa heshima ya Utatu Mtakatifu, ambao ndiyo chanzo cha ukuu wote wa Mama Yetu Bikira Maria. Ibada hii inakusudia kuheshimu Nguvu za Mungu Baba, Hekima ya Mungu Mwana, na Wema wa Mungu Roho Mtakatifu,  kwa ukarimu kwa Mama Yetu Mbarikiwa.

Ibada hii ilifunuliwa na Mama Yetu Bikira Maria mwenyewe kwa mtawa Mbenedikto, Mtakatifu Mechtilde. Katika Kitabu cha Ufunuo wa Mtakatifu Mechtilde tunasoma:

"Wakati Mechtilde alipokuwa akiomba msaada wa Bikira Mtukufu pale saa yake ya kifo itakapofika, Mama Yetu alimtokea na kusema: 'Nitakusaidia hakika. Lakini pia nataka usali Salamu Maria tatu maalumu kwangu kila siku.

'Ya kwanza itakuwa kwa heshima ya Mungu Baba, Ambaye nguvu zake zote ziliinua Roho yangu juu sana kuliko kiumbe kingine chochote kwamba, baada ya Mungu, mimi nina nguvu kubwa zaidi mbinguni na duniani. Katika saa yako ya kifo, nitaitumia nguvu hiyo ya Mungu Baba kuweka mbali nguvu yoyote ya giza.

'Salamu Maria ya pili itasaliwa kwa heshima ya Mungu Mwana, Ambaye alinipa hekima Yake isiyoelezeka. Katika saa yako ya kifo, nitaijaza Roho yako na nuru ya hekima hiyo, ili giza lote la ujinga na makosa litoweke.

'Salamu Maria ya tatu itakuwa kwa heshima ya Mungu Roho Mtakatifu, Ambaye alijaza Roho yangu na tamu ya upendo Wake na huruma. Katika saa yako ya mwisho, nitabadilisha uchungu wa kifo kuwa tamu ya kimungu na furaha."

Mwandishi wa  ufunuo wa Mtakatifu Mechtilde alikuwa ni Mtakatifu Gertrude Mkuu, Alikuwepo wakati Mtakatifu Mechtilde alipokufa na aliona Bwana wetu akimtokea. Baadaye, ufunuo mwingi kuhusu Ibada ya Salamu Maria Tatu ulifunuliwa kwa Mtakatifu Gertrude pia.

Katika Sherehe ya Kupashwa  Habari Bikira Maria  mnamo 1299, wakati  wimbo wa Ave Maria ulipokuwa ukiimbwa Kanisani, Mtakatifu Gertrude aliona maono ya miale mitatu ya mwanga iliyokuwa ikitoka  kwa kila nafsi tatu za Utatu Mtakatifu, miale hiyo aliiona ikipenyeza Moyo wa Bikira Mtakatifu, kama miale mitatu. Alielewa kuwa miale mitatu yenye kung'aa ilikuwa alama kwamba: "Baada ya Nguvu za Baba, Hekima ya Mwana, na Huruma ya Roho Mtakatifu, hakuna kinachokaribia Nguvu, Hekima, na Huruma ya Maria."

Kisha aliona miale mingine ikirudi kwenye chanzo chake cha kwanza, na alifunuliwa kujua kwamba hizo zilikuwa neema ambazo Mama Yetu anawapa  wale wanaosali Sala ya Salamu Maria kwa ibada.

Siku nyingine Bikira Maria alimtokea Mt. Gertrude na kusema:

"Kwa nafsi yoyote inayosali Salamu Maria Tatu kwa uaminifu, nitamtokea saa ya kifo katika utukufu wa ajabu sana kwamba nitajaza Roho  ya Mtu huyo na faraja ya mbinguni."

Mtakatifu maarufu Anthony wa Padua alikuwa ni Mmoja wa watu wa  kwanza kufanya Ibada hii ya Salamu Maria tatu na kuzipendekeza kwa wengine, Lengo lake maalumu katika ibada hii lilikuwa kuheshimu Ubikira safi wa Maria na kudumisha usafi kamili wa akili, moyo, na mwili katikati ya hatari za ulimwengu. Baadae watakatifu wengi, kama yeye, walifanya ibada hii. Mtakatifu Leonard wa Port Maurice, mhubiri maarufu (1675-1751), alishauri wasikilizaji wake wote kuzingatia ibada hii. Alitoa sala hizi za Salamu Maria tatu  kama toba katika maungamo, ili kupata neema ya kuepuka dhambi zote za mauti wakati wa mchana au usiku, hasa kwa wale waliokuwa wakipambana na dhambi za uchafu; zaidi ya hayo, aliahidi kwa namna maalum, wokovu wa milele kwa wale wote waliokuwa waaminifu kwa ibada hii.

Baada ya mfano wa watakatifu hao wawili wa Kifrancisko, Mtakatifu Alphonsus Maria Liguori alikubali ibada hii nzuri na kuieneza ibadah ii kwa bidii na nguvu. Alishauri matumizi yake, na hata aliwapa kama toba kwa wadhambi. Ibada hii pia aliizungumzia katika kitabu chake kizuri na maarufu “The Glories of Mary”.

Mmoja wa waeneza ibada hii maarufu alikuwa Mkapuchini, Padre John Baptist wa Blois. Na Ilikuwa kwa sababu ya kazi yake katika kueneza Ibada hii  kwamba Papa Leo XIII alihalalisha ibada hii. Huko Blois alianzisha Kundi linaloitwa "Pia Opera kwa Uenezi wa Salamu Maria Tatu." Ibada hii Iliidhinishwa na Maaskofu wengi, kwa muda mfupi ikawa imeenea katika nchi nyingi. Baadaye, mnamo Julai 30, 1921, Papa Benedict XV, katika barua ya Kitume, aliiinua hadhi ya Ibada hii akiipatia Rehema  nyingi sala hii.

Post a Comment

0 Comments