Machapisho yanayopendwa

6/recent/ticker-posts

MEDALI YA MIUJIZA.

 



Mnamo majira ya saa sita usiku, Mtakatifu Catherine Labouré aliamshwa na sauti laini, ikisema, "Sista,sista, sista." Matukio ya kimiujiza yalimpeleka kwenye kikanisa ambapo Bikira Maria alitokea na kuketi karibu na Altare ya kikanisa hicho. Mtakatifu Catherine alipiga magoti miguuni pake, akaweka mikono yake mikononi mwa Maria, akamtazama machoni, na kufanya mazungumzo ya moyo kwa moyo naye.

Miezi minne baadaye, mwezi wa Novemba mwaka 1830, Maria alitokea tena kwa Mtakatifu Catherine katika Kikanisa hicho kilichochopo Rue de Bac. Wakati huu, Mama yetu Mtakatifu alikuwa amesimama juu ya duara, na miali ya mwanga wa kung'aa ikitoka kwenye mikono yake iliyotandazwa. Karibu na Mama Mara kulikuwa na maandishi: "Ee Maria, Mkingiwa dhambi ya asili, utuombee sisi tunakuomba." Maria aliposema na Mtakatifu Catherine, alisema,  "Tengenezeni medali kwa mfano huu. Wale wanaoivaa watapokea neema kubwa, hasa wakiivaa shingoni. Wale wanaoisoma sala hii kwa unyenyekevu watakuwa, kwa njia ya pekee, chini ya ulinzi wa Mama wa Mungu. Neema zitamiminika kwa wingi kwa wale wanao amini."

Kwa idhini ya Kanisa Katoliki, medali za kwanza zilitengenezwa mwaka 1832 na kusambazwa Paris, nchini Ufaransa. Inajulikana kuwa medali kumi za awali zipo, na mojawapo inahifadhiwa kwenye Shrine  la Medali ya Miujiza.



Kwa haraka zaidi, baraka ambazo Maria aliahidi zilianza kuonekana kwa wale waliokuwa wakivaa medali yake, na hivi Ufaransa yote watu walianza kuita medali huo "Medali wa Miujiza." Matumizi ya Medali yalisambaa kutoka nchi hadi nchi, na wakati wa kifo cha Mtakatifu Catherine mwaka 1876, medali zaidi ya bilioni moja zilikuwa zimetengenezwa. Mpaka Leo, Medali bado inavuta baraka kutoka kwa Mungu kwa mwili na roho.

MAANA YA MEDALI YA MIUJIZA.

Medali ya Miujiza awali ilijulikana kama Medali ya Bikira Maria Mkngiwa dhambi ya asili, lakini, kutokana na  miujiza mingi kutoka kwa wale waliokuwa wakivaa, watu walianza kuipa jina la Medali ya Miujiza, na jina likabaki. Medali hii ni kumbukumbu ya kuona ya wokovu wetu kupitia Yesu Kristo.

Upande Wa Mbele.



Upande wa mbele wa Medali ya Miujiza unaonyesha Maria Mkingiwa dhambi ya asili, mikono yake ikiwa wazi, imejaa mwanga. Mtakatifu Catherine Labouré alimwona Bikira Maria akionekana hivi na kumsikia akisema, "Tengenezeni medali kufuatana na mfano huu. Kila mtu atakayevaa shingoni atapokea neema kubwa." Maria anasimama juu ya duara kama Malkia wa Mbingu na Dunia. Miguu yake inaonekana ikiwa imekanyaga  nyoka kuashiria kwamba Shetani na wafuasi wake wote ni dhaifu mbele zake (Mwa. 3:15). Kumbukumbu ya "Bikira Maria kuumbwa bila dhambi" inaunga mkono dogma ya Kukingiwa kwake Bikira Maria dhidi ya dhambi — Dogma hii inamuelezea Maria kuwa  “asiye na dhambi”, "amejaa neema," na "amebarikiwa miongoni mwa wanawake wote" (Lk. 1:28). Dogma ya Bikira Maria kukingiwa dhambi ya asili ilitangazwa miaka 24 baadaye mwaka 1854, na kuthibitishwa wakati Maria alipotokea kwa Mtakatifu Bernadette Soubirous huko Lourdes, Ufaransa, mwaka 1858.

Upande Wa Nyuma.



Kwenye upande wa nyuma, Msalaba na herufi M zinaashiria uhusiano wa karibu wa Maria na mateso, na kifo cha Mwana wake. Msalaba unaweza kuashiria Kristo na ukombozi wetu, na mstari chini ya msalaba ni ishara ya ardhi na Altare, kwa sababu ni kwenye Altare wakati wa Misa kwamba sadaka ya Kalvari inaendelea kuwepo duniani leo. M inamaanisha "Maria" na "Mama." Uunganishaji wa herufi za mwanzo za Maria na msalaba unaonyesha ushiriki wa karibu wa Maria na Yesu na ulimwengu wetu. Hapa, tunaona jukumu la Maria katika wokovu wetu na jukumu lake kama Mama wa Kanisa.

Chini ya Msalaba, mstari, na M kuna mioyo miwili iliyoko upande mmoja: Moyo Mtakatifu wa Yesu uliovikwa miiba na Moyo Immakulata wa Maria uliopenywa na upanga. Mioyo miwili inawakilisha upendo wa Yesu na Maria kwetu.

Nyota kumi na mbili zinaashiria kabila kumi na mbili za Israeli na mitume kumi na mbili, wanaowakilisha Kanisa lote wanavyomzunguka Maria. Pia inakumbusha maono ya Mtakatifu Yohane, mwandishi wa Kitabu cha Ufunuo (12:1), ambapo "ishara kubwa ikaonekana mbinguni, mwanamke amevikwa jua, na mwezi chini ya miguu yake, na juu ya kichwa chake taji ya nyota kumi na mbili."

Karibu kuvaa Medali ya Miujiza, alama ya neema na ulinzi kutoka kwa Bikira Maria. Medali hii ni kumbukumbu ya upendo wa Yesu na Maria kwetu na ni chanzo cha baraka tele. Kama vile Mtakatifu Catherine Labouré alivyoagizwa na Bikira Maria, kuvaa medali hii ni kujitia chini ya ulinzi wa Mama wa Mungu na kupokea neema kubwa. Kwa mujibu wa ahadi ya Maria, wale wanaoivaa watapata ulinzi maalumu na baraka tele. Jiunge nasi katika kuvaa Medali ya Miujiza, kuwa karibu na neema zinazotokana na upendo wa Mungu kupitia Bikira Maria.

Post a Comment

0 Comments