Maneno
ya Bwana Yesu: “Leo niletee roho za watu wenye uaminifu na uchaji wa Mungu,
na uwazamishe katika Bahari Kuu ya Huruma yangu. Roho za watu hawa ndizo
zilizonifariji katika njia ya Msalaba. Wao ndio waliokuwa tone lile la faraja
nilipokuwa katikati ya bahari ya uchungu na mateso.”
Tuwaombee
watu wote waaminifu na wenye ibada ambao walimtuliza Yesu katika mateso yake.
Ee Yesu
mpole na mwenye huruma sana, Wewe huchota neema kwa wingi kutoka katika hazina
Yako, na kuzigawa kwa ukarimu kwa kila mmoja wetu na kwa watu wote. Tunakuomba
utupokee katika makao ya Moyo wako mpole na wenye huruma nyingi, na usituache
tutoroke humo kamwe. Tunakuomba neema hii, kwa ajili ya mapendo ya ajabu,
yawakayo moyoni mwako kwa Baba yako wa mbinguni. Amina
Baba
yetu … Salamu Maria … Atukuzwe …
Baba wa
Milele, elekeza macho yako yenye huruma, kwa watu wote walio waaminifu, kama
vile kwenye hazina na urithi wa Mwanao. Kwa ajili ya mateso yake ya
kuhuzunisha, uwajalie Baraka zako, na ulinzi wako daima. Kwa njia hii, waweze
kuimarika katika upendo, na wala wasije wakapoteza hazina bora ya Imani Tashi
Takatifu, bali, pamoja na majeshi yote ya malaika na watakatifu, waweze kuisifu
na kuitukuza huruma yako isiyo na mwisho, kwa milele yote. Amina
1 Comments
Good God bless you
ReplyDelete