Machapisho yanayopendwa

6/recent/ticker-posts

NOVENA YA HURUMA YA MUNGU SIKU YA TANO.

 


Maneno ya Mkombozi: “Leo niletee roho za ndugu waliojitenga na Kanisa, na uwazamishe katika Bahari Kuu ya Huruma yangu. Wakati ule wa mateso yangu makali, watu hawa waliurarua mwili wangu na roho yangu, yaani Kanisa langu. Pindi warudipo tena katika Umoja wa Kanisa, majeraha yangu hupona, na kwa njia hii wanapunguza ukali wa mateso yangu”.

Tuwaombee wale waliopotoka katika Imani Katoliki na kujitenga na Kanisa.

Ee Yesu Mpole na mwenye Huruma, Wewe u Huruma na Wema wenyewe, hukatai kuwapa mwanga wale wote wanaoutafuta. Uzipokee ndani ya Moyo wako wenye Huruma, roho za ndugu zetu waliojitenga. Uwavute kwa mwanga wako, ili warudi tena katika Umoja wa Kanisa lako Takatifu, na uwadumishe humo, wasiweze kutoroka tena Moyo wako wenye Huruma sana, bali uwawezeshe wao pia pamoja nasi, kuusifu na kuutukuza ukarimu wa Huruma Yako Kuu, kwa milele na milele. Amina.

Baba yetu … Salamu Maria … Atukuzwe …

Baba wa Milele, uzielekee kwa macho ya huruma, roho za ndugu zetu waliojitenga na Kanisa lako Takatifu, hasa wale waliozitapanya Baraka zako na kuzitumia vibaya neema zako, kwa kuendelea kishupavu katika mafundisho yao ya upotofu. Usiyaangalie hayo makosa yao, bali uutazame upendo wa Mwanao Mpenzi, pamoja na mateso yake makali aliyovumilia kwa ajili yao. Watu hawa pia, wameingizwa ndani ya Moyo wa Yesu Mwanao, wenye Huruma Kuu. Uwawezeshe vile kwamba, wao pamoja na sisi sote, tuisifu na kuitukuza Huruma Yako Kuu, kwa milele na milele. Amina

Post a Comment

0 Comments